VPL: AZAM YAIBURUZA MBEYA CITY NYUMBANI, MTIBWA YASHIKWA.

Michezo mingi ya ligi kuu Tanzania bara imechezwa leo katika viwanja tofauti tofauti,Azam walikuwa mjini Mbeya kuvaana na Mbeya City katika mchezo uliokuwa mkali na wenye ushindani wa hali ya juu sana ila wameweza kuibuka na ushindi mdogo wa bao 1-0 ambalo limepachikwa kimiani na nahodha wao Aggrey Moris.
Matokeo  ya michezo mingine ni Morogoro derby kati ya Mtibwa Sugar na Polisi ya Morogoro ambazo zimetoka nguvu sare bila ya kufungana.
Na huko mkoani Mtwara katika uwanja wa Nangwanda timu ya Ndanda FC imekubali kichapo cha mabao 3-1  toka kwa JKT Ruvu. Mabao ya JKT Ruvu yalifungwa na Juma Ndeule, Abrahman Mussa na Thomas Matayo.

0 comments:

Post a Comment