TIMU YA JULIO YAKWAMA KUINGIA LIGI KUU.

 
 
Pamoja na kikosi chake cha Mwadui kushinda mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Daraja la Kwanza dhidi ya Polisi Dodoma lakini Mwadui imeshindwa kupanda Ligi Kuu Bara.

Ushindi huo uliifanya Mwadui inayonolewa na Julio kufikisha pointi 31 ambazo zingeipandisha lakin Stand United iliyoshinda mabao 2-1 dhidi ya Toto Afrika, ikafikisha pointi 29.

Lakini mwisho kabisa, Stand United ikabebwa na rufaa yake dhidi ya Kanembwa ikafikisha pointi 32, na moja kwa moja ikapanda Ligi Kuu Bara.
Kama si rufaa, Julio alikuwa amerejea Ligi Kuu Bara, hali iliyofanya uongozi wa Mwadui kulalama kuhusiana na pointi hizo za rufaa.

0 comments:

Post a Comment