Nahodha mpya wa Brazil, Neymar Jr ameonyesha
uungwana wa kimichezo baada ya kukubali kumsamehe beki Juan Zuniga wa Colombia.
Zuniga ndiye aliyemuumiza kwa kumvunja
Neymar Jr mfupa mdogo wa mgongo na kumfanya aondolewe kwenye michuano ya Kombe
la Dunia hatua ya robo fainali.
Lakini katika mechi ya kirafiki ya timu hizo
juzi mjini Miami, Marekani ambayo Brazil ilishinda bao 1-0, Neymar alizungumza
vizuri na Zuniga na baadaye kumkumbatia.
Hali hiyo ilionyesha kiasi gani ameamua
kumsamehe na alimsalimia tena baada ya mchezo.
Mechi hiyo ilikuwa ni ya kwanza kwa Neymar
kupewa unahodha na Kocha Mpya, Dunga. Colombia nao wakampa Zuniga unahodha wa
mechi hiyo.
Wanamichezo wengi wamemsifia Neymar Jr kwa
kuonyesha ukomavu huo.
0 comments:
Post a Comment