ARGENTINA WAWAFANYA MBAYA UJERUMANI-DI MARIA SHUJAA

WINGA Angel di Maria ametengeneza mabao matatu na kufunga moja, Argentina ikilipa kisasi cha Kombe la Dunia kwa kuifunga 4-2 Ujerumani usiku huu katika mchezo wa kirafiki mjini Dusseldorf, Ujerumani.
Mchezaji huyo ghali zaidi kuwahi kusajiliwa Manchester United na Uingereza nzima alipika mabao ya Sergio Aguero, Erik Lamela na Federico Fernandez kabla ya kufunga na lake mwenyewe siku 52 tangu bao la Mario Gotze katika muda wa nyongeza liipe Ujerumani ubingwa wa dunia nchini Brazil.
Mabao matano kati ya sita yamefungwa na wachezaji wa Ligi Kuu ya England, huku Andre Schurrle akiifungia Ujerumani kabla ya Gotze kuwafungia bao la pili mabingwa hao wa dunia. 


Kifaa halisi; Angel di Maria ameng'ara vilivyo leo Argentina ikilipa kisasi cha Kombe la Dunia kwa Ujerumani


CREDITS:BONGOSTAZ.COM

0 comments:

Post a Comment