Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara Azam leo wameanza
safas\ri asubuhi na basi lao jipya kuelekea Mbeya kwa ajili ya mpambano
mkali wa ligi kuu katika uwanja wa Sokoine siku ya Jumamosi hii.
Azam wameondoka wakiwa na kikosi cha wachezaji 20, huku afisa habari
wa Azam Jaffer Idd amewataja wachezaji ambao hawajaondoka sababu bado
hawajawa fiti ni Bocco, Friday na Mwantika ambao sasa wameanza mazoezi
mepesi, Domayo naye pia ameanza kujifua na goti limeanza kukunja lakini
Kimwaga yeye bado kabisa.
Azam wameamua kuondoka mapema leo ili wapate siku za kupumzika na vile vile kufanya maandalizi ya mwisho na kuzoea mazingira.
Mabingwa hao watashuka uwanjani wakiwa na pointi saba na wako katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi wakati nafasi ya nne inashikiliwa na wenyeji hao Mbeya City.
Credits:Kandanda.
0 comments:
Post a Comment