LIGI KUU ENGLAND: MANCHESTER UNITED VS WEST BROMWICH

Ligi kuu ya Uingereza inatarajiwa kuendelea usiku wa leo huku Manchester United wakiwa ugenini kupambana na West Bromich Albion katika mchezo utakao kuwa mkali na kusisimua.
Manchester United wanaingia uwanjani wakiwa wameshinda michezo miwili mfululizo ikiwemo mchezo dhidi ya West Ham 2-1, Everton 2-1.
West Bromich wanaingia uwanjani wakiwa kwenye fomu nzuri ila tu hawana rekodi nzuri na michezo ya nyumbani dhidi ya Manchester United, katika michezo 18 ya mwisho West Bromich ameweza kufungwa michezo 13.
Manchester United itaingia uwanjani huku ikimkosa nahodha wao Wayne Rooney kwa sababu ya kutumikia adhabu yake ya kadi nyekundu,upande mwingine wachezaji Chris Smalling  Ander Herrera, Ashley Young, Phil Jones and Michael Carrick wameendelea kufanya mazoezi leo na wachezaji wenzao kwa maandalizi ya mchezo wa leo.

0 comments:

Post a Comment