Ligi ya Ungereza imeendelea tena wiki hii kwa michezo mingi
na viwanja tofauti huku vinara wa ligi hiyo kwa sasa Chelsea wamezidi
kujichimbia kileleni baada ya kuwachapa Crystal Palace kwa mabao 2-1.
Chelsea walianza kwa moto sana na kuweza kupata bao la mapema mnamo
dakika ya 6 ya mchezo kupitia kwa mshambuliaji wao Oscar.Dakika ya 40
mlinzi wa Chelsea Ceser Azpilicueta alipata kadi nyekundu sambamba na
Damien Delaney mlinzi wa Crystal Palace nae alipata kadi nyekundu baada
ya mwanzo kuwa na njano moja.Mpaka mapumziko Chelsea walikuwa wanaongoza
kwa bao 1-0 huku timu zote wakicheza wakiwa 10.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Chelsea wakionekana kuwa bora
na kusaka ushindi,jitihada zao zilizaa matunda baada ya kiungo wao
mwenye kiwango cha juu sana Cesc Frabregas kupachika bao la 2 kwa
Chelsea,Chelsea walizidi kutawala mpira kwa asimia kubwa sana ila dakika
ya 90 ya mchezo Crystal Palace walipata bao la kufutia machozi kupitia
kwa Fraizer Campbell.
Matokeo mengine katika ligi hiyo ni Washika bunduki wa London Arsenal
nusu kudondokea pua katika uwanja wa nyumbani baada ya kupata sare ya
2-2 dhidi ya Hull City,Southampon wamefanya kufuru kubwa baada ya
kuibuka na ushindi wa rekodi ya mabao 8-0 dhidi ya Sunderland,Everton
3-0 Aston
Villa,Newcastle 1-0 Leicester City,Burnley 1-3 West Ham na
Manchester City 4-1 Totten Ham Spurs.
0 comments:
Post a Comment