SIMBA VS YANGA HAKUNA MBABE

kubwa iliyokuwa mioyoni mwa watu wengi juu ya mchezo wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga imekwisha leo kwa timu hizo kushindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 0-0.
Katika mchezo huo kila timu iliingia uwanjani kwa presha kubwa ya kupata ushindi dhidi ya mwenzake,huku timu ya Simba ikiingia uwanjani na kipa namba tatu na chipukizi Manyika kutokana na kuumia kwa makipa wao Ivo Mapunda na Casillas,Manyika alionekana kuwa bora zaidi katika mchezo huo na kushangaza watu uwanjani uwanjani kwani hawakutegemea kumuona akiwa katika ubora huo.
Kipindi cha kwanza cha mchezo Simba walionekana kuwa bora zaidi huku mshambuliaji Okwi akionekana kuwa mwiba katika nafasi ya ulinzi ya Yanga.Kipindi cha pili cha mchezo huo mambo yalikuwa kinyume baada ya Yanga kurudi mchezoni na kuonekana kuwa bora zaidi ya Simba ila ubora wao uliishia hivyo hivyo hawakuweza kupata bao lolote.
Hadi kipenga cha mwisho cha mchezo matokeo yalibaki kuwa 0-0.

CREDIT:SALEH JEMBE/ KANDANDA TZ.

0 comments:

Post a Comment